MTUHUMIWA WA MAUAJI YA KAMANDA AELEZA WALIVYOJIFICHA MAKABURINI BAADA YA KUFANYA MAUAJI
Abdurahman Ismail aka Dulla (28) ambaye ni
mkazi wa Mkudi Ghana jijini Mwanza ambaye ni mdogo wa watuhumiwa Muganyizi
Michael Peter aliyedaiwa kumfyatulia risasi marehemu Barlow alieleza jinsi
walivyo tekeleza unyama wao na kwenda kuficha radio call na funguo za gari kwa
kutupa katika tankila maji taka katika eneo la Nyashana kwenye nyumba ambayo
haina mahusiano yoyote na hao watuhumiwa bali kwa lengo la kuhakikisha vitu
hivyo havipatikani kabisa.
Watuhumiwa wawili waliofungwa pingu wakiwa
wameshikiliwa na makachero wa jeshi la polisi waliovalia kiraia wakiwaonyesha
kwenye shimo la maji taka eneo ambalo walitupa Radio call pamoja na funguo za
gari la aliyekuwa Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza marehemu Liberatus
Barlow.
Watu hao walitumbukiza radio call hiyo na
funguo za gari kupitia bomba linaloonekana kulia la kupitishia hewa ya maji taka
na hapa ni harakati za kutindua mlango wa shimo la maji taka lililotajwa kuwa na
radio call na ufunguo wa gari la vilivyokuwa vikitumiwa na marehemu Barlow siku
ya tukio la mauaji yake eneo la minazi mitatu Kitangili wilayani Ilemela jijini
Mwanza.
Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Mkoa wa
Mwanza (RCO) Joseph Konyo akijiandaa kuchungulia ndani ya shimo la maji taka
lililotajwa kuwa na radio call na ufunguo wa gari la vilivyokuwa vikitumiwa na
marehemu Barlow siku ya tukio la mauaji yake eneo la minazi mitatu Kitangili
wilayani Ilemela jijini Mwanza.
Picha ya ndani ya shimo hilo..
Funguo za gari zikifanyiwa usafi..
Hivi ni baadhi ya vitu vilivyokamatwa nyumbani
kwa watuhumiwa hao vikiwemo vyeti vya kughushi, pasipoti na picha za
utambulisho wa kughushi wa kipolisi, simu zaidi ya nne zenye laini zake na laini
nyingine za ziada kwa mitandao tofauti, sare za moja kati ya makampuni ya ulinzi
Mwanza, kofia zenye nembo ya jeshi la Polisi na kadhalika...
No comments:
Post a Comment