Monday, January 28, 2013

MWANZA'S PER CAPITA INCOME UP

 Mwanza Region has achieved great success in the poverty alleviation campaign, recording an increase of its residents per capita income from Sh421, 379 in 2005 to Sh924, 536 by June 2012.     
The region’s seven-year development report shows that the residents’ income has gone up by 219 per cent.    
The report on the region’s economic achievement was released  by the Mwanza Regional commissioner, Eng Everist Ndikilo, at his year-end meeting with the media and experts from several government departments in the region.    

“The increase, which is approximately Sh2,500 per day, means that Mwanza residents are far above the poverty line pegged at below $1 (Sh1,500), explained Eng Ndikilo.    

Further, Mr Ndikilo said, agriculture has remained the leading sector in the region by producing more than 75 per cent of its income.    

Fishing, one of the leading sectors, earned the region seven per cent of its income. According to him, it also recorded a big increase from Sh1.34 billion in 2005 to Sh3.38 billion this year.

“This is also a good sign that Mwanza Region is becoming a force to reckon with in the development and investment sectors with an increase of 251 per cent,” explained the RC.    

Once a dusty town, in recent years Mwanza has emerged an economic giant in the country.    

Credit for the achievement is shared mainly by the government through creative plans and a no-nonsense approach towards whoever dares mess up things and a responsive business community.    

Founded in 1892 by a German colonial administrator, Emin Pasha, as a centre for coordinating cotton exports, Mwanza has finally seen its bright future as investors scramble for a stake in it.    

This is mainly thanks to the booming Nile Perch industry, mining sector and cotton farming.    

What used to be home to thousands of squatters and dusty roads has today become a haven of skyscrapers, modern gardens, well built roads and robust economic activities.         

Friday, January 25, 2013

MTUHUMIWA WA MAUAJI YA KAMANDA AELEZA WALIVYOJIFICHA MAKABURINI BAADA YA KUFANYA MAUAJI

Abdurahman Ismail aka Dulla (28) ambaye ni mkazi wa Mkudi Ghana jijini Mwanza ambaye ni mdogo wa watuhumiwa Muganyizi Michael Peter aliyedaiwa kumfyatulia risasi marehemu Barlow alieleza jinsi walivyo tekeleza unyama wao na kwenda kuficha radio call na funguo za gari kwa kutupa katika tankila maji taka katika eneo la Nyashana kwenye nyumba ambayo haina mahusiano yoyote na hao watuhumiwa bali kwa lengo la kuhakikisha vitu hivyo havipatikani kabisa.

Watuhumiwa wawili waliofungwa pingu wakiwa wameshikiliwa na makachero wa jeshi la polisi waliovalia kiraia wakiwaonyesha kwenye shimo la maji taka eneo ambalo walitupa Radio call pamoja na funguo za gari la aliyekuwa Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza marehemu Liberatus Barlow.

Watu hao walitumbukiza radio call hiyo na funguo za gari kupitia bomba linaloonekana kulia la kupitishia hewa ya maji taka na hapa ni harakati za kutindua mlango wa shimo la maji taka lililotajwa kuwa na radio call na ufunguo wa gari la vilivyokuwa vikitumiwa na marehemu Barlow siku ya tukio la mauaji yake eneo la minazi mitatu Kitangili wilayani Ilemela jijini Mwanza.

Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Mkoa wa Mwanza (RCO) Joseph Konyo akijiandaa kuchungulia ndani ya shimo la maji taka lililotajwa kuwa na radio call na ufunguo wa gari la vilivyokuwa vikitumiwa na marehemu Barlow siku ya tukio la mauaji yake eneo la minazi mitatu Kitangili wilayani Ilemela jijini Mwanza.

                                               Picha ya ndani ya shimo hilo..

                                          Funguo za gari zikifanyiwa usafi..

Hivi ni baadhi ya vitu vilivyokamatwa nyumbani kwa watuhumiwa hao vikiwemo vyeti vya kughushi, pasipoti na picha za utambulisho wa kughushi wa kipolisi, simu zaidi ya nne zenye laini zake na laini nyingine za ziada kwa mitandao tofauti, sare za moja kati ya makampuni ya ulinzi Mwanza, kofia zenye nembo ya jeshi la Polisi na kadhalika...

 

Tuesday, January 15, 2013

MEYA WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA AVUNJA REKODI KWA KUVUNJA MIPAKA YA SIASA



Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ambaye pia ni diwani wa kata ya Kitangiri Henry Matata akihutubia wananchi katika uwanja wa wazi wa Kitangiri jijini Mwanza uliokuwa na lengo la kuwasilisha shughuli za utendaji wa kata yake sambamba na kufafanua mikakati iliyopo juu ya masuala mbalimbali ya maendeleo kwenye kata hiyo.




Meya wa Ilemela henry Matata ambaye pia ni diwani wa kata ya Kitangiri jijini Mwanza ameapa kupambana kufa na kupona kutatua suala sugu la migogoro ya ardhi ambalo limeendelea kuwa kero ndani ya wilaya yake akiwaasa pia wananchi wa wilaya ya Ilemela kufuata utaratibu wote stahili hasa linapokuja suala la ununuzi au umiliki wa ardhi.


Awali vijana wanaomshabikia Meya Henry Matata waliingia viwanjani hapo kwa mbwembwe wakitokea makaburini ambako walishiriki mazishi ya mmoja kati ya mwanamtaa aliyefariki dunia kwa mapenzi ya mola katani humo.



Suala lililovunja rekodi ndani ya mkutano huo wa hadhara ni hatua ya Meya huyo wa Ilemela kupitia CHADEMA kuvunja mipaka ya itikadi za siasa kwa kualika viongozi na wanachama wa vyama vyote huku akiwaachia kujimwaga na sare zao na hata nyimbo zao za vyama vyao ila tu kwa masharti ya kutohusisha kauli za kubezana zinazoweza kuleta chokochoko hali inayoweza kupelekea uvunjifu wa amani.





Shabiki nambari moko....


Wataalamu mbalimbali kutoka ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela nao walialikwa kwenye kusanyiko hili kwaajili ya kutoa ufafanuzi wa utekelezaji pindi maswali yapapo tokea..

Meya ameahidi kuendelea kuhamasisha wananchi wa Kata ya Kitangiri kushiriki kuhamasisha wadau mbalimbali kuchangia ujenzi wa shule za sekondari hivyo kuondoa uhaba wa vyumba vya madarasa unaoziandama shule nyingi kwa sasa.
                                                                   source:gsengo blog

Monday, January 14, 2013

TUSONGE PAMOJA TENA 2013

Imekuwa kitambo toka mwaka jana kabla ya kusimama kidogo ku post different issues "STRICTLY MWANZA"Naomba mniuwie radhi kwa kimya,sasa nimerudi'so beautiful people 2013 sio mwisho but the begining of a new AGE...!Happy new year.